Habari
Polepole ajibu baada ya kuambiwa viatu vya Nape vinampwaya
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole baada ya Mbunge wa Iringa mjini , Mchungaji Peter Msigwa kumwambia kitendo cha Msukuma kumkumbuka Nape ni ujumbe tosha kuwa viatu vya Nape vinampwaya.
Hata hivyo nae Polepole hakukaa kimya baada ya tweet hiyo nae aka jibu hivi “Kitu kimoja nakuahidi, hii ni term yako ya mwisho, tunakurudisha kufanya kazi ya Uchungaji maana naona mchungaji anajichanganya na mbuzi,” alijibu Pole Pole.
Mara nyingi kiongozi huyo wa CCM amekuwa akijibu hoja mbalimbali katika ukurasa wake wa Tweeter ambapo wadau mbalimbali huuliza maswali na yeye hujibu kwa mfumo wa tweet.
Na Emmy Mwaipopo