Michezo

Polisi Arusha watuma salamu za vitisho kwa Uhamiaji

Timu ya netiboli ya Polisi mkoani Arusha imepanga kuwavua ubingwa klabu ya Uhamiaji wakati wa mashindano ya kusaka klabu bingwa ya Tanzania Bara yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 13 mwaka huu jijini Arusha.
Timu ya Netiboli, Polisi Arusha

Uhamiaji ni bingwa mara tatu wa mashindano hayo yatakayofanyika kwenye Uwanja wa Sheik Amri Abeid, ambapo mkoa wa Arusha utawakilishwa na timu tatu za Polisi, Madini na Arusha City Queens.

Kocha wa Polisi Arusha, Emerciana Silas amesema nafasi ya wenyeji waliyopewa wataitumia vizuri kuhakikisha ubingwa unabaki hapo ili kuonyesha klabu zingine za mikoani kutoa fikra kuwa kombe hili si la mkoa wa Dar es Salaam

Mwaka huu sisi ndio wenyeji na tunataka kuonyesha wenyeji wetu kwa timu tutakazochuana nazo kuwa tuko nyumbani na hao walioshikilia kombe miaka yote wajiandae kuliachia, niseme tu kuwa kimazoezi tuko vizuri na tunafanya hapa hapa, hivyo kwa mwaka huu hakuna jipya chini ya jua tutakalolishindwa na uzuri mbinu zao (Uhamiaji) hivyo kikubwa kwa sasa wadau wa Arusha waje washuhudie tunavyochukua kombe,” amesema Silas kwenye mahojiano yake na gazeti la Mwananchi.

Kwa upande mwingine Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA), Anna Kibira amesema wameamua kuyapeleka mashindano hayo mkoa wa Arusha ili kutoa fursa kwa timu wenyeji kujaribu bahati yao ya kupoka ubingwa wa Uhamiaji.

By Godfrey Mgallah

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents