Habari
Poromoko la barafu juu ya hoteli laua makumi Italia
Poromoko kubwa la barafu limeanguka kwenye hoteli ya kifahari nchini Italia baada ya kutokea tetemeko la ardhi. Maafisa wamesema Alhamis hii kuwa takriban watu 30 wamefunikwa.
Miongoni mwa waliofukiwa ni wafanyakazi na wageni wa hoteli hiyo ya iitwayo Rigopiano ya mjini Farindola. Hadi sasa mwili mmoja umeokolewa.