Burudani
Post Malone king’ang’anizi chati za Billboard
Bado Post Malobne amekaa namba moja katika chati za muziki za Billboard Hot 100 kupitia ngoma yake ya ‘Rockstar’ aliyomshirikisha rapper 21 Savage.
Post ambaye anafanya vizuri pia katika vituo vingine vya runinga kupitia ngoma hiyo ameshikilia namba moja kwa takribani wiki mbili mfululizo katika chati hzio mama duniani za muziki.
Namba mbili inashikiliwa na Camila Cabello ft kupitia ngoma yake ya ‘Havana’ aliyomshirikisha Young Thug, wakati Ed Sheeran Duet anashikiria namba tatu kupitia ngoma aliyomshirikisha mwanadada Beyonce iitwayo ‘Perfect’.
Lil Pump anashikiria namba nne kupitia ngoma yake ya ‘Gucci Gang’ na ngoma ya ‘Thunder’ kutoka kwa Imagine Dragons ikikamata namba tano.