Prezzo kuiteka Dar April 5
Kwa mara ya kwanza mfalme wa kunyuka pamba kali Afrika Mashariki, Jackson Makini aka Prezzo anatarajia kuwasha fire jijini Dar es Salaam Ijumaa hii.
Show hiyo itafanyika kwenye ukumbi wa New Maisha Club ambapo mashabiki wake watamshuhudia The Masai Warrior akiperform hit song zake zikiwemo Nateta Action, For sure 4 shizzle, Ma city Ma town na zingine kibao.
Show ya Prezzo itasindikizwa na wasanii kibao wa Bongo huku kiingilio kikiwa ni shilingi 10,000 kawaida na shilingi 20,000 kwa VIP.
Show ya Prezzo imeandaliwa na kampuni ya Unity Entertainment.