MichezoUncategorized

Professa Jay ana haya ya kuiambia Simba SC

Legendari wa Muziki wa kizazi kipya nchini na Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule , “Professa Jay” ameitaka timu yake ya Simba kuweka nguvu zaidi katika fainali ya kombe la shirikisho kuliku kombe la ligi.

      Legendari wa Muziki wa kizazi kipya , Joseph Haule , “Professa Jay”.

 

Simba SC ipo katika nafasi ya pili katika ligi kuu soka Tanzania Bara ikiwa na alama 62 sawa na klabu ya Yanga inayoongoza kwa tofauti ya Mabao, pia ikiwa na michezo mitatu mkononi.

Professa Jay licha ya kuiombea timu yake kutwaa Ubingwa wa ligi kuu, amesema Simba ina nafasi ya kuutwaa Ubingwa wa kombe la shirikisho watakapocheza fainali dhidi ya Mbao FC kwenye uwanja Wa Jamhuri mjini Dodoma  May  28.

Professa Jay ambaye ni Mbunge wa Chadema kupitia jimbo la Mikumi, alisema ubingwa wa Ligi Kuu kwa Simba utatagemeana na mechi za Yanga, kama watashinda mechi zao 3 zilizobaki watajihakikishia ubingwa huo tofauti na Simba yenye mechi mbili itakuwa ni kazi bure hivyo ni vyema zaidi kujipanga kwa fainali ya FA.

Furaha yangu ni kuona Simba Sc inachukua ubingwa wa ligi kuu bara na ubingwa wa shirikisho, kutokana na ubora wa kikosi cha timu yetu hivyo tutashinda mechi zilizobaki na kutwaa ubingwa, japo imani yangu kubwa zaidi ipo kwenye kombe la shirikisho. “alisema Professa Jay”.

BY HAMZA FUMO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents