Habari
Professor Jay na mrembo Victoria Kimani ‘ngoma inogile’, wenyewe wasema yajayo yanafurahisha
Kama wewe ni shabiki wa Rapa Professor Jay kaa mkao wa kula kwani kuna bonge la kolabo na time hii amevuka boda hadi Kenya na kumvuta mrembo Victoria Kimani.
Professor Jay kupitia ukurasa wake wa Instagram, ameweka picha inayomuonesha kama wapo location na kuiandikia maneno yaliyosomeka “Yajayo YANAFURAHISHA, WATCH yatapita video kwenye BIO, Tukifikisha Malengo yetu TUNAFUMUAAA Tena“.
Hii itakuwa ni kolabo ya kwanza kwa Professor Jay ndani ya mwaka huu ambayo amefanya na msanii kutoka nje ya Tanzania.