Michezo

Pweza mtabiri ageuzwa kitoweo baada ya kuibashiria Japan kipigo

Wakati michuano ya kombe la dunia ikiwa inaendelea nchini Urusi, Pweza aliyekuwa anaaminika katika kubashiri matokeo ya mechi kadhaa zilizopita ikiwemo za timu ya taifa ya Japan ameuawa na kugeuzwa kiteo.

Kimio Abe mwenye umri wa miaka 51, akionekana na tabasam huku akishika kichwa cha Pweza Rabio.

Pweza huyo aliyekuwa akifahamika kwa jina la Rabio amejizoelea umaarufu mkubwa kwenye michuano hiyo kutokana na umahiri wake katika kubashiri mshindi wa mechi husika.

Mmiliki wa Pweza huyo ambaye ni mvuvi anayetambulika kwa jina la Lakini Kimio Abe amesema kuwa ameamua kumuuza na kugeuzwa kitoweo kwakua amebaini kuwa atajizoelea kitita cha fedhe kuliko kama angeendelea na utabiri ambao hauja mnufaisha licha kupatia.

Rabio predicted that Poland would beat Japan yet the football team appeared to remain involved longer than the eight-limbed mollusc

Licha kugeuzwa kitoweo, Rabio ambaye alikuwa Pweza mkubwa amefanikiwa kuibashiria Japan kupata kipigo dhidi ya Colombia na hata sare yao dhidi ya miamba ya soka ya Afrika timu ya taifa ya Senegal.

Baada ya kuibashiria Japan kufungwa dhidi ya Ubelgiji hatua ya 16 bora Pweza huyo hakuweza kushuhudia utabiri wake ukitimia kutokana na kuingizwa sokoni.

Abe ambaye ndiyo mmiliki wa Pweza huyo amesema yupo Pweza mwingingine ambaye ataendelea kubashiri michano hiyo inayoendelea nchini Urusi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents