Burudani

Q Chief azungumzia kwanini ngoma zake hazifanyi vizuri pamoja na mapungufu ya label ya Q Mhonda

Msanii mkongwe wa muziki Q Chief amedai kuwa kuna mambo ambayo anakosea kwenye muziki wake ndiyo maana ngoma zake kadhaa alizoziachia hivi karibuni zimeshindwa kufanya vizuri zaidi kama alivyotarajia.

Q Chief akiwa na Mkurugugenzi wa Qs Mhonda Entertainment

Muimbaji huyo ambaye yupo chini ya label ya Qs Mhonda Entertainment, ameiambia Bongo5 kuwa hali hiyo imemfanya akae yeye pamoja na uongozi wake ili kulitafuta ufumbuzi suala hilo.

“Baada ya kufanya ngoma kadhaa nimeona kuna ulazima wa kukaa chini na uongozi wa management yangu na kuisukuma ijisukume zaidi kunisukuma kwa maana thamani ya uwekezaji wa audio na video unatakiwa kuwa sawa au zaidi na thamani na promotion pamoja na maisha halisi ya msanii ambayo anatakiwa kuishi,” alisema Q Chief.

Aliongeza, “Kwa hiyo mwaka 2017 ni mwaka ambao nataka kufanya mabadiliko makubwa sana, lakini kabla ya yote nataka marekebisho katika mkataba wangu na Q Mhonda kwa sababu una mapungufu mengi sana, na ningependa kuyarekebisha kwa lengo la kuweka mambo sawa,”

Pia muimbaji huyo amewashukuru mashabiki wa muziki wake kwa kuonyesha mapokezi mazuri katika wimbo wake mpya alioshirikiana na Patoranking wa Nigeria.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents