Q Chillah kuwa chini ya menejimenti ya Rwanda
Msanii wa muziki nchini, Q Chillah amesema anabadili management yake kutoka Tanzania hadi Rwanda ili kutanua muziki wake Kimataifa zaidi.
Akizungumza na bongo5 jana, Q chillah amesema yupo kwenye makubaliano ya mwisho na management mpya ya Rwanda ambayo itamsimamia muziki wake.
“Katika hatua ambazo nazifanya kubadili muziki wangu na kufika mbali zaidi kimataifa,nimebadili management kutoka Tanzania to Rwanda. Kwahiyo sasa hivi tuna mawasiliano mazuri na Rwanda kuhusu hili suala nadhani soon nitaweka wazi baada ya makubaliano ya mwisho.Wakati mwingine inabidi uhame daraja lile ambalo upo, muziki umebadilika tunatakiwa twende na wakati,sio nani anasema nini?,nani amehoji? Mimi sitaki kujua mimi ninachotaka kujua ni dunia inataka nini kwenye muziki wangu na kufanya muziki bora,” alisema.