“Bado mimi na Saidi Fellah” – King Kiboya
Anayejulikana kama Meneja wa kundi la Wanaume Halisi bwana King Kiboya kwa jazba kubwa sana baada ya kuona vijana wake wanakamua ile mbaya alibahatika kukutana na mwandishi wa Mtandao huu na kumtaka aweke wazi kwa wasomaji…
Anayejulikana kama Meneja wa kundi la TMK Wanaume Halisi bwana King Kiboya Kwaito kwa jazba kubwa sana baada ya kuona vijana wake wanakamua ile mbaya alibahatika kukutana na mwandishi wa Mtandao huu na kumtaka aweke wazi kwa wasomaji kuwa anahitaji yeye kama yeye kupambana na Meneja wa TMK Wanaume kivyovyote vile.
Shughuli ya vijana wangu inaonekana jinsi ilivyokuwa ya kufa mtu sasa hiyo ni ngoma ya vijana sasa nataka kuwaonesha kuwa na mimi mtu mzima nimo namtaka Fellha Jukwaani tupimane msuli King Kiboya Kwaito.
Mameneja wa makundi haya wamekuwa na sifa moja ambayo humfanya kila mtu kuvutiwa nao, kwani wanapokuwa kazini urafiki huwekwa kando lakini katika mazingira ya kawaida huonekana kuwa ni kitu kimoja tena maswahiba wa karibu sana.