Burudani
Quick aja na Bambataa
Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Abbott Charles ‘Quick rackers Anatarajia kutoka upya na video na wimbo wa Bambataa ambao ameimba tofauti na staili anayoitumia.
Akazungumza na safu hii mwanamuziki huo ambaye anavuma kwa staili ya Kranka ya kuimba haraka zaidi, na hata mashairi yake kuwa ya kigumu kwa sasa anakuja na staili ambayo hajawahi kuitumia popote.
Aidha anasema amejaribu kutumia staili hiyo kutoka na wimbo wenyewe ni wakucheza zaidi , na pia anataka kuonyesha jamii kwamba yeye ni mkali na anaweza kubadilika kwa kila staili.
“Wimbo huo nahitaji kwanza nianze kuutambulisha kwenye tv, na ndipo nimalizie kwenye video” alisema Rackar ambaye alitamba sana katika wimbo wa Bullet na kisa sio pombe wa Mwasiti.