Michezo
Radamel Falcao asajiliwa rasmi na Chelsea
Mabingwa wa ligi kuu ya England, Chelsea wamekamilisha dili la kumsajili mshambuliaji wa Colombia, Radamel Falcao kwa mkopo wa mkataba wa muda mrefu kutoka Monaco, huku kinda wa Blues Mario Pasalic akihamia upande mbadala kama sehemu ya makubaliano.
Falcao mwenye miaka 29 ambaye mkataba wake uko Monaco, alikuwa analipwa £285,000 kwa juma Old Trafford, lakini sasa amepunguziwa mpaka £140,000 akiwa Stamford Bridge.
Mshambuliaji huyo alikuwa na msimu mbaya alipokuwa Manchester United kwa mkopo piaA. Alifunga magoli manne tu katika mechi 26.