Michezo
Rafael da Silva aondoka Man United, ajiunga na Lyon ya Ufaransa
Manchester United imemuuza beki wa kulia, Rafael da Silva mwenye umri wa miaka 25 kwenda Lyon ya Ufaransa. Mchezaji huyo alijiunga na United akiwa na pacha wake Fabio kutoka Fluminense mwaka 2008.
Klabu ya Lyon ya Ufaransa imekamilisha usajili wa beki huyo kwa mkataba wa miaka minne na kwa kitita ambacho hakikutajwa.
Kupitia Twitter, mchezaji huyo aliandika: Nataka kuwashukuru mashabiki kwa mapenzi kwa miaka minane niliyokuwepo hapo.”
Rafael amecheza jumla ya michezo 170 na kufunga mabao matano huku pacha wake Fabio alijiunga na Cardiff City katika msimu wa 2014.