Michezo
Rafael Nadal atolewa mashindano ya Tenisi ya ATP na Cuevas
Mcheza Tenisi Rafael Nadal jana ameshindwa kuingia katika hatua ya Nusu Fainali ya mashindano ya Tenisi ya ATP baada ya kupoteza mchezo kwa seti tatu kwa Mruguay Pablo Cuevas katika mashindano ya wazi ya Rio.
Bingwa huyo wazamani mara 14 wa Grand Slam alianza kwa kuongoza kwa pointi mbili kwa seti mbili lakini baadaye alianza kupoteza mchezo kwa kufungwa jumla ya 6-7 (6) 7-6 (3) 6-4.
Nadal pamoja na kupoteza mchezo huo amesema amekubali kushindwa na atajaribu kulifanyia kazi na kubadili mwelekeo.
Cuevas ambaye anashikilia nafasi ya 45 ulimwenguni atakutana na Guido Pella katika hatua ya fainali.