Michezo
Rafael Nadal atupwa nje michuano ya ATP London
Mchezaji wa tennis namba moja duniani Rafael Nadal ametupwa nje katika michuano ya fainali za ATP mjini London.
Nadal amepokea kichapo hiko cha seti 7-6 7-5 6-7 4-7 6-4 Jumatatu hii kutoka kwa David Goffin ambaye anashika namba saba duniani.
Picha ya David Goffin ambaye amemtoa Rafael nadal kwenye mashindano ya ATP mjini London
Hata hivyo Nadal aliingia katika mchezo huo akiwa na majeraha ambayo yalikuwa yakimsumbua tangu alipokuwa katika michuano ya Paris Masters.