Habari

Raia wa Italia aliyetekwa nyara Kenya aachiliwa huru 

Raia wa Italia Silvia Romano aliyetekwa nyara nchini Kenya miezi 18 iliyopita ameachiliwa huru.

Akizungumza kupitia shirika la habari la serikali, RAI, waziri wa mambo ya nje wa Italia Luigi Di Maio amesema kuwa Romano alipatikana nchini Somalia.

Hata hivyo, hakutoa maelezo zaidi kuhusu kuachiliwa kwake japo gazeti la Corriere della Sera limeripoti kuwa Italia ililipa kikomboleo ili aachiliwe.
Waziri Mkuu wa Italia Giuseppe Conte ameshukuru vikosi vya ujasusi vya nje kwa usaidizi wao kwa kupatikana kwa Romano.
Maafisa nchini Kenya hawajatoa tamko lolote kuhusu kuachiliwa Mtaliano huyo. Mnamo Novemba mwaka 2018, watu waliokuwa wenye silaha walimteka nyara Romano aliyekuwa akifanya kazi na shirika la misaada la Africa Milele.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents