Raia wenye hasira waushambulia kwa mawe msafara wa Rais Museveni, Mbunge wa upinzani ‘Bobi Wine’ akamatwa kwa uchochezi
Msafara wa Rais wa Uganda, Yowel Musevani jana Agosti 13, 2018 mjini Arua umeingiwa na dosari baada ya moja ya gari lililokuwa kwenye msafara huo kubondwa na mawe.
Vyombo vya habari nchini Uganda vimeripoti kuwa vurugu hizo zilizuka baada ya askari polisi kuanza kuwafyatulia risasi mamia ya watu waliokuwa wakiandamana kupinga kitendo cha polisi mjini Arua kumpiga risasi Dereva wa Mbunge wa Upinzani, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine.
Police has shot my driver dead thinking they've shot at me. My hotel is now coddoned off by police and SFC. #Arua pic.twitter.com/fw0GeV0vU9
— BOBI WINE (@HEBobiwine) August 13, 2018
Jeshi la Polisi mjini Arua kupitia kwa msemaji wake, Emilian Kayema amethibitisha taarifa hizo na kudai kuwa watu kadhaa wanashikiliwa na polisi akiwemo Bobi Wine.
Hata hivyo jeshi hilo limekataa kuweka bayana kama watu hao ni miongoni mwa waandishi wa habari ambao nao usiku wa jana walikamatwa na kupelekwa kusikojulikana hadi hivi sasa.
Rapa Bobi Wine ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kyyadondo yupo mjini Arua kumpigia kampeni rafiki yake anayegombania Ubunge kwa mwavuli wa vyama vya upinzani, ambapo jana pia Rais Museveni alienda huko kumnadi mgombea ubunge wa chama chake.
Chanzo: Reuters
No Comment! Siasa za afrka ni hatare!
No Comment! Siasa za afrka ni hatare!
stupidity gonvement