Rais Donald Trump apendekeza uchaguzi wa urais uahirishwe
Donald Trump ametoa wito kuwa uchaguzi wa rais utakaofanyika Novemba uahirishwe akidai kuongezeka kwa upigaji kura kwa njia ya posta kunaweza kusababisha udanganyifu na matokeo yasiyo sahihi.
Kuna ushahidi mdogo wa madai ya Bwana Trump lakini kwa kipindi kirefu amekuwa akipinga upigaji kura kwa njia ya posta ambao anadai unaweza kusababisha udanganyifu, huku akiongeza kuwa endapo hayo yatatokea itakuwa ni aibu kwa taifa kama Marekani, ameongeza kuwa anashauri uchanguzi uahirishwe akiamini kuwa utakuwa safi na salama.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter Rais Donald Trum ameandika ujumbe huu:-
With Universal Mail-In Voting (not Absentee Voting, which is good), 2020 will be the most INACCURATE & FRAUDULENT Election in history. It will be a great embarrassment to the USA. Delay the Election until people can properly, securely and safely vote???
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) July 30, 2020