Habari
Rais Kenyatta ahutubia taifa kwa majonzi ‘magaidi wameuawa ila tumewapoteza wenzetu 14’ (+video)
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta leo Januari 16, 2019 amelihutubia Taifa hilo kufuatia tukio la shambulizi la kigaidi lililotokea siku ya jana katika Hoteli ya Dusit D2, huko Westlands, Jijini Nairobi.
Rais Kenyatta amesema kuwa mpaka sasa watu 14 wameuawa na kudai kuwa magaidi wote waliohusika kwenye tukio hilo wameuawa usiku wa jana.