Rais Magufuli afanya uteuzi mdogo, Waziri Kairuki ahamishwa Wizara (+video)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo amefanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na kuteua Mawaziri, Makatibu wakuu na Balozi.
Kwenye mabadiliko hayo, aliyekuwa Waziri wa Madini Mhe. Angela Kairuki amehamishwa na kuwa Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu / Uwekezaji.
TAZAMA ORODHA KAMILI HAPA CHINI:
Angela Kairuki – Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu/Uwekezaji
Dotto Biteko – Waziri wa Madini
Stanslaus Nyongo – Naibu Waziri Madini
Joseph Nyamhanga – Katibu Mkuu TAMISEMI
Zainabu Chaula – Katibu Mkuu Afya
Elius Mwakalinga – Katibu Mkuu Ujenzi
Doroth Mwaluko – Katibu Mkuu Sera
Doroth Gwajima – Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI
Francis K Michael – Naibu Katibu Mkuu UTUMISHI
Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amefungua Ubalozi mpya wa Tanzania nchini Cuba ambao utakuwa katika mji wa Havana, na Balozi wake atatangazwa hivi karibuni.