Habari

Rais Magufuli aitangaza Dodoma kuwa Jiji

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameutangaza rasmi Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji kama ilivyokuwa baadhi ya mikoa ikiwemo Dar es Salaam.

Rais Magufuli amelitangaza hilo leo wakati wa sherehe za miaka 54 ya Muungano zinazofanyika kwenye uwanja wa Jamuhuri mkoani Dodoma.

“Kuanzia leo kwa mamlaka mliyonipa Dodoma ni jiji. Dodoma ni Jiji. Na Mkurugenzi wa hapa kuanzia leo anakuwa Mkurugenzi wa jiji la Dodoma,” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo Mhe. Magufuli amesisitiza wananchi wa Zanzibar na Tanzania Bara kuulinda vizuri Muungano huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents