Habari
Rais Magufuli aitumbua bodi ya wakurugenzi ya TRA na mwenyekiti wake
Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mamlaka ya mapato nchini TRA, Bernard Mchomvu ameamka na habari mbaya Jumapili hii. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli amemshushia rungu yeye na bodi yake.
Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ikulu Jumapili hii:
Hatua hiyo imekuja katika kipindi ambacho mamlaka hiyo imeonesha kufanya vizuri zaidi katika kukusanya mapato ambapo imefanikiwa kukusanya shilingi trilioni 1.15 kwa mwezi Oktoba mwaka huu ikiwa ni kukamilisha malengo waliyojiwekea katika ukusanyaji wa mapato.