Habari
Rais Magufuli amtaka Prof. Muhongo kujiuzulu
Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli leo amemtaka Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kwa kushindwa kusimamia wizara yake.
Rais Magufuli amesema hayo baada ya kamati iliyokuwa ikichunguza suala la mchanga kwenye makontena kukabidhi ripoti yao.
“Nina mpenda Profesa Muhongo na lakini pia ni rafiki yangu, lakini kwenye hili aji asses na bila kuchelewa nilitaka aachie madaraka,” amesema Rais Magufuli.
Akikabidhi ripoti hiyo, Profesa Mruma amesema uchunguzi huo umebaini uwepo wa madini ya kiasi cha kati ya Shilingi 829.4 bilioni mpaka 1.439 Trillioni kwa makontena yote 277.
Na Emmy Mwaipopo