Habari

Rais Magufuli ampongeza Rais Kenyatta kwa ujenzi wa barabara ya kisasa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta wamezindua barabara ya Southern Bypass huku Rais Magufuli akisema wananchi wanahitaji maendeleo na hayo ndio yenyewe.

14915571_1440392175989331_5633888333426358079_n

Akizungumza katika sherehe hiyo, Rais Magufuli amempongeza Rais Kenyatta na serikali yake kwa kujenga barabara hiyo ambapo amesema haitawasaidia wananchi wa Kenya tu, bali pia itawasaidia wananchi wa Afrika Mashariki wanaotumia barabara zinazopitia Nairobi.

“Wananchi wanahitaji maendeleo na haya ndio maendeleo, barabara hii itasaidia kuinua uchumi na itasaidia masuala ya kijamii,” alisema Rais Magufuli.

Barabara hiyo ina urefu wa kilometa 28 na inaunganisha maeneo mbalimbali ya jiji la Nairobi. Uzinduzu huo umefanyika katika eneo la Karen nje kidogo ya jiji la Nairobi.

Hizi ni baadhi ya picha katika ufunguzi wa barabara hiyo:

3

5

6

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents