Rais Magufuli amtumia salamu za pongezi Rais Mteule wa DR Congo, Felix Tshisekedi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za pongezi Rais Mteule wa DR Congo, Felix Tshisekedi kwa kutangazwa na mahakama nchini humo kuwa ndiye mshindi wa nafasi ya urais kwenye uchaguzi uliofanyika Desemba 30, 2018.
Rais Magufuli ametuma salamu hizo kupitia ukurasa wake wa Twitter, ikiwa ni siku moja imepita tayari tangu Mahakama nchini humo, kufuta malalamiko ya baadhi ya wagombea wenza wa Tshisekedi kudai kuwa matokeo ya uchaguzi yaligubikwa na wizi.
Felix Tshisekedi anakuwa Rais wa kwanza kutoka katika chama cha upinzani nchini humo, na ameshinda kwa asilimia 38 ya kura zote zilizopitwa kwenye uchaguzi huo.
Soma zaidi –http://bongo5.com/felix-tshisekedi-atangazwa-rasmi-na-mahakama-kuwa-rais-mteule-wa-dr-congo-01-2019/