Habari

Rais Magufuli amuaga mgeni wake Kenyatta, ampa zawadi hii pia wameteta mambo haya kuhusu maendeleao ya mataifa ya Afrika Mashariki (+ Video)

Rais Magufuli amuaga mgeni wake Kenyatta, ampa zawadi hii pia wameteta mambo haya kuhusu maendeleao ya mataifa ya Afrika Mashariki (+ Video)

Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Muigai Kenyatta tarehe 06 Julai, 2019 amerejea nchini Kenya baada ya kumaliza ziara yake binafsi ya siku 2 aliyomtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Wilaya ya Chato Mkoani Geita.


Kabla ya kuruka katika uwanja wa ndege wa Chato, Mhe. Rais Kenyatta amefanya mazungumzo ya faragha na mwenyeji wake, Mhe. Rais Magufuli katika Kijiji cha Mlimani na baada ya mazungumzo hayo viongozi hao wamezungumza na waandishi wa habari.

Viongozi hao wamesema mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano wa Tanzania na Kenya hususani katika masuala ya kiuchumi ambapo wametaka biashara baina ya nchi hizo ikuzwe zaidi pamoja na kujenga uwiano wa kibiashara wenye maslahi kwa pande zote.


Mhe. Rais Magufuli amesema kwa kuzingatia kuwa Kenya imefanya uwekezaji mkubwa zaidi nchini Tanzania ikilinganishwa na uwekezaji wa Tanzania nchini Kenya, wamekubaliana kuwa kampuni za Kenya zijielekeza kuongeza thamani ya bidhaa kwa kuanzisha viwanda vitakavyosindika mazao na kuchakata bidhaa mbalimbali hapahapa Tanzania badala ya kusafirisha malighafi kwenda Kenya.
Ameongeza kuwa wamekubaliana kuwa Kenya itanunua gesi ya Tanzania badala ya kuagiza kutoka nje ya Bara la Afrika kwa kuwa Tanzania imejaaliwa gesi nyingi, na wamewaagiza Mawaziri wa Tanzania na Kenya kukutana na kujadili namna Kenya itavyonunua gesi hiyo.


Kuhusu ziwa Victoria ambalo kwa asilimia 51 lipo Tanzania na kwa asilimia 5 lipo Kenya, Mhe. Rais Magufuli amesema wamekubaliana kuwa Mawaziri wa nchi hizo wahakikishe meli za Tanzania na Kenya zinaimarishwa na kuondoa vikwazo vinavyokwamisha meli hizo kufanya kazi ya kukuza biashara katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda ambazo zinazunguka ziwa hilo.


Kwa upande wake, Mhe. Rais Uhuru Kenyatta amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa mapokezi mazuri aliyoyapata hapa Chato, na kwa upendo mkubwa uliooneshwa na wananchi wa Chato kwake na ujumbe wake, na ameeleza kuwa huo ni uthibitisho wa uhusiano mzuri, undugu na urafiki wa karibu wa Wakenya na Watanzania.
Amesema pamoja na kuimarisha zaidi uhusiano wa Tanzania na Kenya uliojengwa na Waasisi wa Mataifa hayo.

By Ally Juma.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents