Habari

Rais Magufuli apokea hati za utambulisho wa mabalozi watano

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt John Pombe Magufuli leo jumanne tarehe 01 Agosti 2017 amepokea hati za utambulisho wa mabalozi watano kutoka katika nchi walizotumwa kuja kuziwakilisha nchini.

Mabalozi waliowasilisha hati zao kwa Rais Magufuli ni Nguyen Kim Doahu Balozi wa Vietnam, Prof Ratlan Pardede Balozi wa Indonesia, Mwadhama Askofu Mkuu Marek Solenski Balozi wa Vatican, Dkt Detlef Wachter Balozi wa Ujerumani na Balozi Richard Tumisiime Kabonero kutoka Uganda.

Pitia Taarifa kamili kutoka Ikulu

By Godfrey Mgallah

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents