Habari

Rais Magufuli atoa onyo kwa makampuni ya simu nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametahadharisha kuwa, wapo mbioni kuhakikisha mapato ya serikali yanadhibitiwa zaidi ili taifa liweze kujitegemea kikamilifu, huku akionya makampuni ya simu nchini.

Rais Magufuli ameyasema hayo Ijumaa hii, mjini Dodoma wakati akikabidhiwa taarifa ya vyeti feki. Rais ameyaonya makampuni hayo, akisema, dawa ya makampuni hayo bado inatengenezwa.

“Bado kuna maeneo mengi ambayo tunaibiwa fedha. Kwenye haya makampuni ya simu haya, yanafanya transactions nyingi lakini hela haziingii serikalini, dawa yao tunaitengeneza baada ya muda mfupi kidogo itakamilika,” alisema Rais Magufuli huku akishangiliwa.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents