Habari

Rais Magufuli awapongeza wajumbe wa kamati za Makinikia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amekutana na wajumbe wa kamati zilizofanya uchunguzi wa mchanga wa madini huku serikali ikiahidi kuzifanyia kazi taarifa zilizotolewa na kamati hizo.

Rais Magufuli ameyaeleza hayo kupitia taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu leo.

“Timu hiyo imefanya kazi nzuri na yenye maslahi makubwa kwa Taifa na kwamba Serikali itahakikisha inafanyia kazi taarifa zilizotolewa na kamati hizo,” imeeleza taarifa hiyo.

Kamati hizo ziliyoongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma na ya pili iliongozwa na Profesa Nehemia Osoro.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents