Habari

Rais Magufuli awataja wafanyabiashara wanaosumbua kwenye sukari

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli ametangaza kupambana na wafanyabiashara wanaohodhi biashara ya sukari ambao hawazidi hata 10.

160509121817_rwanda_floods_10_624x351_bbc

Akizungumza kwenye ufunguzi wa majengo ya NSSF na PPF jijini Arusha jana, rais Magufuli amesema wafanyabiashara hao ndiyo walishiriki kuviuwa viwanda na kujitajirisha binafsi.

“Wafanyabiashara hawa walinunua viwanda vya NMC wakafungua mashine na kwenda kuuza Msumbiji na wakisimama utawasikia CCM oyee,” aliongeza.

Rais Magufuli amesema atapambana na wafanyabiashara hao bila ya kujali ni wafuasi wa CCM, Chadema au CUF atalala nao mbele kwa mbele.

Aidha Magufuli aliendelea kusema, “Utakuta Watanzania tunaendeshwa na wafanyabiashara kati ya watano au kumi tu, ukienda kwenye sukari ni hao hao, walioua viwanda ni haohao, nawahakikishia nitalala nao mbele hadi mwisho.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents