Habari
Rais Magufuli, Dkt. Kikwete waambatana Afrika Kusini kushuhudia tukio la kuapishwa Ramaphosa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameambatana na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete kuelekea Afrika Kusini kwaajili ya kuhudhuria tukio la kuapishwa kwa Rais mteule wa Taifa hilo, Cyril Ramaphosa.
Rais Ramaphosa anatarajiwa kuapishwa kesho Jumamosi Mei 25, 2019. Hii ni baada ya kuibuka na ushindi wa uchaguzi mkuu uliofanyika mapema mwezi huu.