Habari
Rais Magufuli: Hata corona ikikaa miaka 10, sitashindwa kuwalipa walimu (Video)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Chama Cha Walimu Tanzania-CWT.
Mkutano huo utafanyika katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma, huku watu wote wakitakiwa kuzingatia na kuchukua tahadhari za kujikinga na Virusi vya Corona vinavyosababisha ugonjwa wa Covid-19.
Tayari, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa-Takukuru, Mkoa wa Dodoma, imetangaza kuwa itashughulika na watu watakaojihusisha na vitendo vya rushwa katika Uchaguzi huo.