Habari
Rais Magufuli na TUCTA wakubaliana haya
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewahakikishia viongzoi wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi (TUCTA) kuwa serikali ya awamu ya tano itaendelea kuimarisha zaidi ushirikiano kati yake na wafanyakazi kwa manufaa ya Taifa.
Rais Magufuli amefanya mazungumzo hayo, Alhamisi hii Ikulu jijini Dar es salaam, sambamba na hilo amesema kuwa pamoja na kuimarisha ushirikiano huo serikali iko tayari kupokea ushauri na maoni yatakayotolewa na vyama vya wafanyakazi wenye lengo la kuboresha maslahi ya wafanyakazi na kuongeza tija kazini.
Hii taarifa yake:
Na Emmy Mwaipopo