Rais Mugabe na mkewe wakalia ‘kuti kavu’ Zanu-PF
Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na mke wake, Grace Mugabe wamekalia kuti kavu na kudondoka ghafla katika nyadhifa ndani ya chama tawala cha Zanu- PF nchini humo.
Mapema leo mchana nchini humo kwenye kikao cha kamati kuu cha Chama hicho kimefikia maamuzi ya kumvua Rais Mugabe wadhifa wa kiongozi mkuu wa Chama cha Zanu-PF na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Makamu wake wa Rais, Emmerson Dambudzo Mnangagwa huku mke wake Grace Mugabe akivuliwa uanachama wa Chama hicho.
Hayo yamejili baada ya hali ya sintofahamu inayoendelea nchini kuhusu mtikisiko wa kisiasa na uchumi nchini humo.
Pitia yaliyoafikiwa kwenye kikao hicho maalumu kama yalivyochapishwa na ukurasa rasmi wa Twitter wa Chama cha Zanu PF.
We have recalled president Mugabe, he is no longer the president of ZANU PF. May he leave with grace.
— ZANU PF (@zanu_pf) November 19, 2017
We have confidence in president Cde Mnangagwa our new leader.
— ZANU PF (@zanu_pf) November 19, 2017
We thank the Zimbabwe Defence Force and you, our people for supporting the necessary process. We also hope that our sovereignty will be respected, this OUR country.
— ZANU PF (@zanu_pf) November 19, 2017