Habari

Rais Trump ashambuliwa mitandaoni kwa kukosea Kiingereza, mwenyewe ajitetea na kuwazodoa wanaomsahihisha

Rais wa Marekani, Donald Trump amejikuta akishikwa na hasira baada ya wanaharakati mitandaoni kumsahihisha makosa ya kisarufi (grammatical Error) na kimaandishi (Typing error) kwenye Tweets zake huku wakimkebehi kuwa hajui hata kuandika kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.

Image result for trump grammatical errors
Donald Trump

Trump ambaye jana Julai 04, 2018 alitwiti mara moja na kisha kufuta twiti hiyo baada ya kushambuliwa kuwa alikosea kuandika, huku akidai mtandaoni kuna vyombo vya habari ambavyo haviangalii anachokifanya bali vinaangalia makosa yake ya kisarufi (grammatical error) mtandaoni.

Nimeshawahi kuandika vitabu bora na vilivyouzwa zaidi, kwa hiyo huwezi kunipima kamwe kwenye uwezo wangu wa kuandika. Hii inaonesha wazi kuwa kuna vyombo vya habari vinatoa habari bandia (Feki) kwa kutumia muda mrefu kutafuta makosa kwenye tweet zangu,“ameandika Trump kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Tweet ya kwanza ya Trump ambayo baada ya masaa machache akaifuta na kutweet tena hapa chini

Hata hivyo wataalamu wa lugha waliendelea kumshambulia Trump kuwa bado Tweet hiyo ilikuwa na makosa na kumsahihisha.

Hii sio mara ya kwanza Rais Trump kushambuliwa mitandaoni kwani mwezi Machi mwaka huu gazeti la Washington Post lilimshambulia kwa makosa ya kimaandishi mtandaoni.

Image result for trump grammatical errors

Image result for trump grammatical errors

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents