Habari

Rais Tshisekedi awasamehe waliopanga njama za kumuua Rais Laurent Kabila

Rais Felix Tshisekedi ametoa msamaha kwa watu 26 waliokuwa wamefungwa jela kwa kupanga njama ya mauaji ya Rais wa zamani wa Nchi hiyo, Laurent Kabila mwaka 2001.

Watu hao walihukumiwa vifo na kwa mujibu wa Mamlaka, baadhi yao wamefariki wakiwa gerezani, lakini hakuna hata mmoja ambaye amenyongwa.

Rais Laurent Kabila aliuawa kwa kupigwa risasi na Mlinzi wake Januari 16, 2001 na muda mchache baadaye, Mlinzi huyo alipigwa risasi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents