Habari

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ahudhuria ‘Listening Party’ ya Miss Karun aliyekuwa member wa Camp Mulla

Aliyekuwa member wa kundi la Camp Mulla Miss Karun jana jioni (August 13) alifanya ‘Listening Party’ ya album yake mpya, na mmoja kati ya wageni waalikwa waliohudhuria ni pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.

karun2

Taarifa ya kuthibitisha juu ya Rais Uhuru Kenyatta angehudhuria party hiyo ilitolewa mapema jana na Dennis Itumbi ambaye ni ‘head of diaspora and new media relations’ katika Serikali ya Kenya, ambaye alitweet “President Uhuru Kenyatta to attend the launch of Miss Karun’s first solo album this evening”. Party hiyo ilifanyika Muthaiga Golf Club, Nairobi.

karun1

Hii ilikuwa ni taarifa njema kwa Karun ambaye pia alitweet kuonesha furaha yake na jinsi ambavyo hakuamini,

Album hiyo itakayozinduliwa Ijumaa hii ndio ya kwanza kwa Miss Karun toka ajiondoe katika kundi la Camp Mulla kwa sababu tofauti ikiwemo ya kujiendeleza kielimu. Rais Uhuru Kenyatta ameonekana kuwa kiongozi ambaye yuko karibu na wasanii wa Kenya toka wakati wa kampeni za urais.

Ni jambo la kutia moyo kwa wasanii wenye vipaji kuona viongozi wa ngazi za juu wanasupport jitihada zao za kukuza vipaji walivyonavyo.

Picha: Nairobi Wire

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents