Habari
Rais wa Tanzania Music Foundation afariki dunia kwa ajali ya gari Dodoma
Aliyekuwa Rais wa Tanzania Music Foundation, Dr Donald Kisanga amefariki usiku wa tarehe 8 jijini Dodoma baada ya kupata ajali ya gari.
https://www.instagram.com/p/CDtf8SLBGHi/
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na rafiki wa marehemu, @e.mbasha amesema mwili wa marehemu utasafirishwa kesho kutoka Dodoma hadi Arusha.
Taarifa hiyo imesema mwili utaagwa siku ya Jumatano katika viwanja wa Sheikh Amri Abeid na baada ya hapo shughuli ya mazishi zitafanyika.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.