Michezo

Rais wa TFF atoa neno kwa mara ya kwanza

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia ametoa shukrani zake za dhati kwa wajumbe wote wa Mkutano Mkuu kwa kumpa dhamana ya kuliongoza soka la Tanzania.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia

Karia pia amewataka wale wote waliyokuwa wakiwania nafasi mbali mbali za uongozi ndani ya shirikisho hilo ambao kura zao hazikutosha katika uchaguzi bado mawazo yao yanahitajika na kushirikiana kwa pamoja  kuhakikisha mchezo wa soka unakwenda mbele.

Kiongozi huyo wa ngazi za juu ndani ya Shirikisho lenye dhamana ya kusimamia mchezo wa mpira wa miguu nchini amewapongeza pia viongozi wenzake waliyofanikiwa kushinda na kuwaomba kushirikiana kwa pamoja wakati huo huo akiwashukuru wadau, Serikali na taasisi zake bila ya kuvisahau vyombo vya habari kwa ushirikiano wao katika kufanikisha zoezi la uchaguzi kwenda salama hadi mwisho.

B y Hamza Fumo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents