Michezo

Rais wa TFF, Wallace Karia atuma salamu za pole Cyprus

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF Ndugu Wallace Karia ametuma salamu za pole kwa Chama cha Mpira wa Miguu Cyprus kufuatia kufariki kwa aliyekuwa Rais wa FA Costakis Koutsokoumnis.

Rais wa TFF Ndugu Karia amesema amepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa kwa kumpoteza mmoja wa viongozi wakongwe wa mpira wa Miguu.

Koutsokoumnis alikuwa muhimiri mkubwa kwa soka la Cyprus na amefariki katika wakati ambao Cyprus na mpira kiujumla ulikuwa unamuhitaji,nimesikitishwa na kifo chake na ninatoa pole kwa familia yake,FA ya  Cyprus,FIFA na familia ya soka kwa ujumla” Alisema Rais wa TFF Ndugu Karia.

Mpaka mauti yanamkuta Koutsokoumnis alikuwa ndio Rais wa FA ya Cyprus na amekuwa kwenye kamati mbalimbali za FIFA akiwa Makamu Mwenyekiti na alianza kutumikia soka la Cyprus tokea mwaka 1990.

Amewahi kuwa Makamu wa Rais wa FA ya Cyprus kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais wa FA hiyo mwaka 2001 nafasi aliyoitumikia mpaka mauti yanamkuta.

Koutsokoumnis amefariki Machi 5, 2018 akiwa na miaka 61 baada ya miezi kadhaa ya kupigana kupona ugonjwa wa kansa uliokuwa unamsumbua.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents