Rais wa UFC afunguka pambano la Mayweather na Conor la mwezi August
Dana White ambaye ni rais wa UFC, amefunguka kuhusu pambano la ngumi litakalo mkutanisha Floyd Mayweather na Conor McGregor Jumamosi ya August 26 mwaka huu.
Rais huyo ameshindwa kumtabiri mshindi wa pambano hilo, lakini amesema pambano hilo litakuwa kubwa na amemtaja Conor ni bondia mzuri anayeweza kupambana na mtu yoyote kutokana na umri wake kuwa mdogo tofauti na Mayweather mwenye umri wa miaka 40.
“I’m not saying Conor McGregor’s going to win. I’m not saying Floyd Mayweather’s going to win. But the reason Conor McGregor’s as big as he is is he’ll fight anybody, anywhere, anytime. He will go after Floyd Mayweather and he will try to knock him out,” amesema White.
Picha ya Rais wa UFC, Dana White
Inadaiwa kuwa Mayweather amelipwa kiasi cha dola milioni 100 kwa ajili ya pambano hilo litakalofanyika mjini Las Vegas.