Habari

Rais wa zamani wa Burundi Jean-Baptiste Bagaza afariki dunia

Rais wa zamani wa Burundi Kanali Jean-Baptiste Bagaza amefariki akitibiwa nchini Ubelgiji.

160504075748_burundimap2

Kanali Bagaza amekuwa akitibiwa kwa muda katika hospitali ya Sainte Elisabeth mjini Brussels.

Kupitia akaunti yake ya Twitter mshauri wa rais wa Burundi, Willy Nyamitwe amethibitishwa kuwa rais huyo wa zamani wa nchi ya Burundi amefariki dunia akiwa nchini Ubelgiji.

Kanali Bagaza aliingia madarakani Novemba 1976 kupitia mapinduzi ya kijeshi na aliondolewa madarakani kupitia mapinduzi mengine yaliyoongozwa na binamu wake Meja Pierre Buyoya Septemba 1987.

Source: BBC

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents