Habari
Rais wa zamani wa Iran Akbar Hashemi Rafsanjani afariki dunia
Rais wa zamani wa Iran na mwanzilishi wa chama cha Islamic Republic, Akbar Hashemi Rafsanjani amefariki dunia Jumapili hii akiwa na umri wa miaka 82 mjini Tehran.
Rafsanjani aliwahi kuwa rais wa nchi hiyo kati ya mwaka 1989 mpaka 1997 na alikuwa akishikilia nafasi muhimu katika siasa za Iran wakati huo huo alikuwa akimuunga mkono Rais wa sasa Hassan Rouhani.
Serikali ya Iran imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kutokana na kifo hicho japo mpaka sasa haijawekwa wazi chanzo cha kifo chake.