Habari
Rais wa zamani wa Israel Shimon Peres afariki dunia akiwa na miaka 93
Waziri mkuu wa zamani wa Israel aliyewahi kuhudumu pia kama rais Shimon Peres amefariki dunia akiwa na miaka 93.
Aliugua kiharusi wiki mbili zilizopita na hali yake ikawa mbaya zaidi ghafla Jumanne hii.
Bw Peres, ambaye alikuwa mmoja wa waliosalia kutoka kwenye kizazi cha wanasiasa waliokuwepo wakati wa kuundwa kwa taifa la Israel mwaka 1948, alihudumu kama waziri mkuu wa nchi hiyo mara mbili na mara moja kama rais.
Shimon Peres ameitumikia nchi hiyo kama waziri mkuu mara mbili na mara moja katika nafasi ya Rais.
Simon pia aliwahi kutunukiwa tuzo ya amani ya Nobel kwa ushiriki wake mkubwa katika harakati za kutafuta suluhu ya mgogoro wa kisiasa baina ya Israel na Palestina mnamo miaka ya 1990.