Msanii milionea nchini Kenya Prezzo hivi karibuni ameweka meno ya dhahabu (grillz) huko marekani yenye thamani $3500
Msanii milionea nchini Kenya Prezzo hivi karibuni ameweka meno ya dhahabu (grillz) huko marekani yenye thamani 3500$, na anadai mastaa kibao akiwemo Bow wow wameweka grillz zao katika sehemu hiyo hiyo ambayo amefanyia yeye.
Prezzo aliwahi kufikia hatua ya kumuofa Alicia Keys atumie mikoko yake ya kifahari alipokuwa Mombasa , lakini demu akatoa nje na kudai hakuja kwa matanuzi bali amekuja kwa ajili ya ishu za misaada.
Huyo huyo Mr President aliwahi kwenda Dubai , maalum kwa ajili ya kukamata mchele tu, na wasanii kundi la G-Unit na kulipia maelfu ya dolari kwa kila saa ambalo alilitumia kuwa na machizi hao.
Source: Bongo5