Burudani

Rapa Drake aikana mimba ya mwanadada huyu

Rapa kutoka Toronto, Canada, na mbaya kwa rhymes kali,Darke amejikuta kwenye wakati mgumu, baada ya mwanamke aliyetambulika kwa jina la Sophie Brussaux kudai ni mja mzito na mimba hiyo ni ya Drake.

Drake na mwanadada huyo walionekana pamoja mwezi wa Januari, kwa wikiendi moja na baada ya hapo, wawili hao walinekana kutokuendelea tena na mahusiano yao. Drake amedai kwamba, Sophie alikua ni mwanamke wa kukodiwa kama muuza ngono na kwamba anajulikana kwa tabia za kujaribu kubambikiza mimba. Drake ameongeza kua hashangai mwanadada huyo kutoa shutuma hizo kwani kutokana na kazi anayoifanya Sophie ya kuuza ngono,sio jambo la kushangaza.

Sophie kwa sasa ameajiri wanasheria wakubwa wawili kutoka mji wa New York kufuatilia na kutetea kesi yake.

Kambi ya Drake imeendelea kukanush vikali taarifa hizo wakidai kwamba wanajua mimba hiyo ni ya rapa mwingine na Sophie anataka tu pesa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents