Burudani
Rapper AKA awaduwaza mashabiki wake
Rapper AKA wa Afrika Kusini amewaachia maswali mengi mashabiki wake.
Msanii huyo usiku wa jana (Ijumaa) ameonekana katikati ya ulingo wa mchezo wa mieleka ya WWE akijigamba mbele ya mabaunsa walioshiba ambao wanaonekana ni hatari kwenye mchezo huo.
Swali la mashabiki ni kuwa rapper huyo ameamua kujiunga na mchezo huo ambao unaonekana ni hatari kwa watu wengi kutotamani kuucheza.
Hata hivyo siyo ulingo ule wa WWE ambao umezoeleka huko Marekani, lakini hii ni WWE ya Afrika Kusini ambapo mchezo huo siku ya jana ulifanyika kwenye uwanja wa Sun Arena, Time Square mjini Pretoria.