Burudani
Rapper mkongwe Marekani Daz Dillinger amchana Kanye West
Huenda kipindi hiki Kanye West ndio amekutana na wakati mgumu kuliko muda wote – Tena karibia watu wote wenye asili ya rangi nyeusi wameonyesha hawamkubali kabisa kutokana na maneno yake aliyotoa kwenye mahojiano siku chache zilizopita.
Rapper mkongwe Delmar Drew Arnaud maarufu kwa jina la Daz Dillinger meshindwa kabisa kumvumilia Kanye na kuamua kuachia ngoma ambayo amemchana.
“I’m saying your name. You know who you are, Kanye, be true to the game,” amerap Daz kwenye wimbo huo.
“You wanna be just like Trump. But Trump is calling you a ni**er, you dumb fuck. You can’t pass / Trying to get lipo with your black ass,” ameongeza rapper huyo.