Rappers/waimbaji 10 wa Bongo wenye mbwembe (swag) waongeapo redioni/TV
Uongeaji ni sanaa pia ambapo kuna wale waliojaaliwa uwezo wa kuongea kwa mbwembwe zaidi na kuwa kivutio kwa wanaosikiliza. Hawa ni wasanii 10 tunaoamini kuwa huongea kwa mbwembwe zaidi wahojiwapo redioni ama kwenye TV.
1. Godzilla
Kama haumfahamu Godzilla aka Zizi na hujawahi kumsikia popote, ukifungulia redio na ukakuta anahojiwa unaweza kuhisi ni mnyamwezi fulani aliyekaa Marekani kwa muda mrefu sana na Kiswahili kimeanza kumtoka kichwani. Tangu aanze muziki, Zilla amekuwa akifuata nyendo nyingi za 50 Cent hasa katika kurap na kuongea. Mara nyingi kwenye interview hutupia swag kama za 50 na kwa hakika hakuna anayemfikia.
2. TID
Khalid Mohamed aka Top in Dar huongea kwa kujiamini na dharau kiasi ndani yake (ndivyo alivyo). Katika interview hupenda kuchanganya Kiingereza mara kwa mara ambacho anakimudu poa pia. Mfano mzuri ni kwenye U Heard ya jana ya XXL, Clouds FM kuhusiana na kukwaruzana kwake na Salama Jabir. Mwishoni mtangazaji wa show hiyo Soudy Brown alimuuliza TID anafanya nini maskani, na TID kujibu, “Nipo naangalia tambala moja hivi kwenye 3D kwahiyo I need a lot of attention, I am very sorry can you hang up for me!!”
3. Mr Blue
Blue amepunguza tu mbwembwe siku hizi lakini kama ingekuwa enzi zile, Godzilla asingefua dafu. Blue ni tozi kitambo na ndiye mhasisi wa utamkaji wa maneno ya Kiswahili kwa ladha ya kimombo kwa mfano kabisa itamkwe, kabaisa kitu kilichofanya kuzaliwa kwa aka yake Kabayser.
4. Fid Q
Fid aka Ngosha si mkali tu wa mashairi yenye swagga za moto bali pia hata uongeaji wake. Pamoja na kwamba anatokea Mwanza ambako Kiswahili cha huko kimeathiriwa na kisukuma, Fid huongea kama kashuka jana kutoka states. Uongeaji wake akiwa redioni utadhani ana kigugumizi fulani kumbe ndio swag ziko on. Izingatiwe pia kuwa The Top of Rap’s elite ni profesa wa Kitaalojia.
5. P-Funk
Majani ni muongoezaji mzuri sana redioni. Background yake ya elimu na kutembea sehemu kadhaa duniani, kumemfanya asound kama Mmarekani aongeapo kimombo.
6. Shetta
Shetta aka Bonge la Bwana naye yumo. Anapokuwa akiongea redioni huwa haoni hatari kutupia maneno kadhaa ya kimombo kushtua kidogo.
7. Q Chilla
Chilla ana uongeaji wa taratibu lakini wenye mbwembwe za hapa na pale hasa za kuchomekea viingereza.
8. Izzo B
Uvaaji wa Izzo na uongeaji wake vinaenda sawa. Izzo ni bling blinger na hewani anapokuwa anahojiwa, hit-maker huyo wa Riz-one hutupia swagga kibao na kama anahojiwa na mtangazaji mbovu si ajabu yeye ndio akasound kama mtangazaji wa show, ana vocal kali.
9. Quick Rocka
Quick aka Switcher kama anavyojiita, ni rapper anayeswitch swag kama kinyonga anavyobadili rangi yake. Kama Izzo B, yeye pia ana sauti ya mamlaka hewani.
10. Mo Rocka
Sijui nini kilitokea kwa rapper huyu mtanashati lakini kwa speed aliyokuja nayo kama angekaza, angekuwa mbali. Wakati anaanza kupata umaarufu wengi walikuwa wakimfananisha na Kabayser hasa kwa jinsi anavyorap na hata uongeaji wake kwenye redio.